NGUVU MOJA

NGUVU MOJA

 

Ni mikopo ya vikundi ambayo hutolewa kwa mtu mmoja mmoja (Mwanaume au Mwanamke) anayejiunga katika kikundi cha watu watano wenye biashara endelevu.

 

Sifa za Walengwa

  • Wakazi wa eneo husika ambao wanaendesha na kumiliki biashara halali ndogondogo
  • Wafanyabiashara ndogondogo ambao wako tayari kujiunga kwenye vikundi vya watu watano watano kwa ajili ya kudhaminiana.
  • Wafanyabiashara ndogondogo ambao wanaelewa kuwa deni lolote lazima lilipwe kwa kadri ya makubaliano.
  • Wafanyabiashara ndogondogo ambao wapo tayari kulipa deni pamoja na riba iliyopangwa na benki.
  • Umri usiopungua miaka kumi na nane (18) – (65)

Uundaji wa vikundi

Kikundi kitaundwa kwa hiari na watu wanaofahamiana,Kuheshimiana na kuaminiana, wanaishi jirani na ni wafanyabiashara ambao kwa hiari yao wamekubali kuunda hicho kikundi

  • Kikundi hakitaundwa na ndugu wa familia moja (baba, mama, mke, mume, shangazi, wifi, mke mwenza nk). Iwapo wanafamilia watapenda kujiunga basi wawe kwenye vikundi tofauti.
  • Kikundi kitakuwa na watu watano watano
  • Vikundi vitano hadi sita vya watu watano watano ambavyo vipo katika kitongoji kimoja vitaunda Senta.
  • Kikundi baada ya kuundwa kitasajiliwa na benki kama sharti la kujiunga na mpango wa mkopo.
  • Kila mwanakikukundi atatakiwa kulipa shillingi 5,000 za uanachama wa mpango wa mikopo kwa wafanyabiashara ndogondogo

 

Sifa na Masharti kwa mkopaji

  • Mkopaji lazima awe mwananchama wa kikundi cha watu watano
  • Awe amehudhuria mafunzo ya mikopo yanayotolewa na Benki ya Wananchi kwa muda wa wiki TATU ambapo kila wiki ni siku moja   na kila hiyo siku ya wiki ni muda wa saa moja tu.
  • Mkopo utatolewa kwa mwanakikundi ambaye kikundi chake na senta yake imekubali kumdhamini na kupitisha mkopo wake.
  • Mwanakikundi awe tayari kufanya marejesho ya mkopo kila wiki.
  • Kabla ya kuchukua mkopo mwanakikundi lazima awe ameelewa vizuri kiwango cha kurejesha cha kila wiki cha huo mkopo pamoja na akiba zote za wiki.
  • Mwanakikundi aelewe kuwa baada ya kurejesha mkopo ana haki ya kupata mkopo mwingine.
  • Mikopo itakuwa na vipindi vya marejesho kama ifutavyo:

a.      Mikopo ya Miezi mitatu

b.      Mikopo ya Miezi sita

c.       Mikopo ya Miezi tisa

d.      Mikopo ya Miezi kumi na mbili

e.      Kwa mikopo ya mwanzo 200,000-350,000-500,000 marejesho yatakuwa mwisho miezi sita.

f.        Mwanakikundi atachagua kipindi cha marejesho kwa hiari kulingana na mzunguko wa biashara yake.

  • Mkopaji lazima aweke akiba kila wiki kwa kipindi chote cha mafunzo ya wiki tatu za  mwanzo  akiwa mwanachama wa kikundi. Akiba zinatofautiana kulingana na kiwango cha mkopo unachokopa kwa mfano mkopo wa laki mbili (200,000/=) akiba ni 20,000=, mkopo wa laki tatu na nusu (350,000/=) akiba ni 35,000= na mkopo wa laki tano (500,000/=) akiba ni 50,000=
  • Mwanakikundi atakapochukua mkopo atapaswa kuleta marejesho pamoja na akiba isiyopungua sh.5,000 kila wiki.
  • Mkopaji lazima aweke shilingi 200 kwa wiki kwenye mfuko wa dharura wa senta.
  • Mwanakikundi aelewe kuwa akiba anayoweka ni mali yake na dharura ya shilingi 200 ni mali ya senta.
  • Kila mkopo atakaochukua, mwanakikundi atakatwa bima ya asilimia moja pointi (1.5%) tano ambayo endapo atafariki au kupata ulemavu wa kudumu kama kukatika mikono na miguu deni lake lote litalipwa.
  • Mkopo wa pili na kuendelea utakuwa na ada ya asilimia 3 ya mkopo uliokubaliwa. Ada zitatotelewa na mwombaji kabla ya kupewa mkopo.

 

 

Urejeshaji wa mikopo na uwekaji wa akiba

  • Mikopo yote itarejeshwa na mkopaji kwa mafungu yaliyo sawa kila wiki katika mkutano wa senta.
  • Marejesho ya mkopo yatajumuisha mkopo wenyewe, riba na akiba.
  • Endapo mkopaji atashindwa kuleta marejesho ya wiki, wanakikundi itawabidi wamlipie, iwapo fedha za kikundi hazitoshi, wanasenta itabidi warejeshe. Hiyo ndio maana ya kudhaminiana.
  • Akiba ya kila mwanachama italipia deni endapo wanakikundi au wanasenta wameshindwa kumchangia
  • Kurejesha mkopo halitakuwa suala la hiari wala halina mjadala bali ni lazima
  • Marejesho yataanza mara tu pale mtu atakapochukua  mkopo.
  • Mkopoji anayemaliza deni anahaki ya kukopa mkopo mwingine katika mpangilio ufuatao:

 

Mzunguko wa mkopo kwa awamu

Kiasi cha mkopo

1

200,000 – 350,000-500,000

2

800,000

3

1,000,000

4

1,500,000

5

2,000,000

6

3,000,000

7

4,000,000

8

5,000,000

Muhimu: Mwanakikundi anaweza kuchukua mkopo wa mzunguko wa nyuma kulingana na hali ya biashara kadri anavyoiona na baadae anaweza kurudi katika mzunguko wake wa kawaida hali ya biashara ikiwa nzuri tena.

 

Matumizi ya fedha za mkopo

Mikopo yote itatolewa kwa ajili ya kuimarisha na kukuza biashara ya mkopaji

  • Kutumia mkopo nje ya biashara ni kukiuka maadili ya mkopo
  • Wanakikundi watatakiwa kuhakikisha kuwa waliyemdhamini anatumia mkopo kuimarisha au kukuza biashara ili wasiwe na mzigo wa kumlipia deni endapo atashindwa kurejesha.

 

Kujitoa kwenye mpango au kikundi

kujitoa ni hiari

  • Kabla mwanakikundi hajaamua kujitoa ahahakishe madeni yote yamerejeshwa
  • Endapo wanakikundi wataona mwenzao hafai wanahaki ya kumfukuza lakini kabla hawajafanya hivyo, madeni yote yawe yamerejeshwa.
  • Mwanakikundi kama atakuwa amefukuzwa na wanakundi wenzake benki haitatoa huduma yoyote kwake kwani huduma zote zitapitia kwenye vikundi.

 

Zingatia: Lengo kuu la benki ni kuona biashara ndogondogo zinakua na kuwasaidia walengwa.

   Mkopo lazima urejeshwe  hapatakuwa na sababu yoyote itakayokubaliwa kutokulipa deni.

 

 

Get Help from Our Chatbot
x
ChatBot
Hi 👋! welcome to DCB Chatbot
Powered by The Bridge
This chat session has ended

Thank you for chatting with us, If you can take a minute and rate this chat:

Great
Bad